7.1.2 Asifiksia ya mtoto mchanga

Jinsi ulivyojifunza katika Kipindi cha 4 cha somo, asifiksia ni uhaba wa oksijeni. Asifiksia kwenye uterasi husababishwa wakati ambapo damu ya mama haina oksijeni ya kutosha. Asifiksia kwenye uterasi pia husababishwa na tatizo kwenye plasenta. Asifiksia kwenye uterasi inaweza kusababisha mambo haya:

  • Asifiksia wakati wa kuzaliwa (kidogo, kiasi, au kali).
  • Ugumu katika kusoma au kudhoofika kwa ufahamu. Haya yote huonekana mtoto anapokua. Seli za ubongo huharibiwa kutokana na ukosefu wa oksijeni katika leba na kuzaa.
  • Kifo cha mtoto huyo mchanga.

Mbadilishano wa gesi hutendeka kwa kila pumzi. Oksijeni kutoka kwa hewa iliyovutwa ndani hufyonzwa ndani ya damu inapopita kwenye mapafu. Dioksidi ya kaboni hutolewa kwenye damu hadi kwenye hewa inayotolewa nje.

Hata hivyo, asifiksia ya mtoto mchanga husababishwa na mambo matatu:

  • Mtoto kukosa kupumua baada ya kuzaliwa.
  • Moyo wa mtoto huyo mchanga hauwezi kusukuma damu ya kutosha kwenye mapafu kwa mbadilishano wa gesi.
  • Mtoto huyo mchanga ana viwango vya chini vya hemoglobini (anemia) na kwa hivyo hawezi kutoa oksijeni ya kutosha mwilini mwake.

Mtoto asiyeweza kupumua vyema hawezi kuishi kivyake nje ya mwili wa mama yake. Uhashaji wa mtoto mchanga humsaidia aweze kupumua mwenyewe na kupeleka oksijeni kwenye ogani na tishu zake. Ni lazima ubongo upate oksijeni haraka au uharibike. Unaweza kuhitaji kumhaisha mtoto aliye na anemia kali kutokana na kupoteza damu wakati wa leba na kuzaa. Huenda uhitaji kumhaisha mtoto anayeendelea kuwa na sinosisi hata kama anapumua vizuri. Sinosisi ni ugeukaji wa rangi ya midomo na ngozi kuwa samawati. Sinosisi hutokea wakati ambapo damu haina oksijeni ya kutosha (Picha 7.2).

Picha 7.2 Mtoto aliyezaliwa kabla ya kutimiza muda kamili na mwenye matatizo: Anaonekana mwenye sinosisi (samawati). Mikono na miguu yake ni laini kwa sababu misuli yake ni dhaifu. Ana matatizo ya kupumua. (Picha: Dr Mulualem Gessese)

Ili kuepuka matatizo ya mara moja na ya muda mrefu ya asifiksia, lazima umsaidie mtoto yeyote mchanga asiyeweza kupumua vizuri.

7.1.1 Jinsi mtoto mchanga mwenye afya anavyopumua

7.2 Aina za uhaishaji wa mtoto mchanga