7.2 Aina za uhaishaji wa mtoto mchanga

Jifunze hizi aina tatu za uhaishaji wa mtoto mchanga.

Upitishaji wa hewa safi: Tumia mfuko wa ambu unaotumika kwa mkono (Picha 7.3). Iweke barakoa kwenye pua na mdomo wa mtoto na usukume hewa kwenye mapafu ya mtoto huyo. (Wakati mwingine wataalamu wa afya hutumia neno “uwekaji mfuko wa ambu” kumaanisha upitishaji wa hewa safi.)

Picha 7.3 Mbinu ya kuhaisha ya upitishaji hewa safi ikijaribiwa kwa mwanasesere wa kusomea kwa kutumia mfuko wa ambu. (Picha: Dr Yifrew Berhan)
  • Ufyonzaji: Tumia sirinji ya balbu kuondoa kamasi na viowevu kwenye pua na kinywa cha mtoto.
  • Usingaji wa moyo: Finya kifua cha mtoto kwa mkazo mkali na hafifu ili kuchochea mpigo wa moyo (Picha7.4).
Picha 7.4 Mbinu ya usingaji wa moyo ikijaribiwa kwa mwanasesere wa kusomea. Unaweza kuona chombo cha kupitisha hewa upande wa juu wa kulia wa picha hii. (Picha: Dr Yifrew Berhan)

7.1.2 Asifiksia ya mtoto mchanga

7.2.1 Vifaa vya kimsingi vinavyohitajika kwa uhaishaji wa mtoto mchanga