7.2.2 Kabla ya uhaishaji

Kabla ya kuanza aina yoyote ya uhaishaji, chunguza mambo haya:

  • Ikiwa mtoto yuko hai: Iwapo mtoto mchanga haonekani kuwa hai, kwanza kisikize kifua chake kwa stethoskopu. Usiposikia mpigo wa moyo, mtoto tayari amefariki (Jedwali 7.1).
  • Ulitambua kiwango cha asifiksia. Ikiwa unaweza kusikia mpigo wa moyo, lakini unaukadiria kuwa chini ya mipigo 60 kwa dakika, kwanza msinge moyo. Kisha, pitisha hewa safi ukisita na kuendelea, hadi mipigo ya moyo iwe zaidi ya 60 kwa dakika (Jedwali 7.1).
  • Mtoto hajachafuliwa na mekoniamu: Iwapo mtoto amechafuliwa na mekoniamu (Picha 7.5), kwanza fyonza kwenye kinywa, pua na maeneo ya koromeo. Au iwapo kaviti za kinywa na pua zimejaa kiowevu chenye mekoniamu (Picha 7.5), kwanza fyonza kwenye kinywa, pua na maeneo ya koromeo. Upitishaji wa hewa hufanya tatizo kuwa baya zaidi. Upitishaji wa hewa huingiza kiowevu chenye mekoniamu kwenye mapafu ya mtoto. Kiowevu kwenye mapafu huzuia mbadilishano wa gesi.
Picha 7.5 Mtoto huyu hapumui. (Kifua na pua havisongi.) Mekoniamu iko kwenye mwili wote. (Picha: Dr Mulualem Gessese)

7.2.1 Vifaa vya kimsingi vinavyohitajika kwa uhaishaji wa mtoto mchanga

7.3 Tathmini kiwango cha asifiksia