7.3 Tathmini kiwango cha asifiksia

Watoto walio na asifiksia kiasi au kali wanahitaji huduma makini ya uhaishaji. Jifunze jinsi ya kutambua kiwango cha asifiksia kwa mtoto mchanga. Tathmini kama mtoto yuko hai au amefariki katika sekunde 5 baada ya kuzaliwa. Iwapo yuko hai, kadiri kiwango cha asifiksia. Huenda mtoto aliye na asifiksia kali asipumue kabisa. Hasongezi mikono wala miguu yake. Rangi ya ngozi yake ni samawati sana au nyeupe sana. Mtoto asiyeweza kupumua au anayetweta ili kupata hewa anahitaji huduma ya dharura. Mtoto anayepumua chini ya pumzi 30 kwa dakika pia anahitaji huduma ya dharura. Mtoto asipopumua punde tu baada ya kuzaliwa, ubongo wake unaweza kuharibika au kufariki. Ukiwahaisha watoto vizuri na kwa haraka, wengi wao wanaweza kuongoka.

Jedwali 7.1 linaorodhesha mambo utakayochunguza ili kutathmini kiwango cha asifiksia kwa mtoto mchanga. Pia, tazama picha za watoto wachanga walio na viwango tofauti vya asifiksia (Picha 7.1, 7.2 na 7.5).

Mtoto mchanga anayetweta anaweza tu kuvuta pumzi chache na kwa ugumu. Mitweto mikubwa kati ya kila pumzi pia ni tatizo. Mtoto mchanga anayetweta, kwa kawaida huwa karibu kufariki.

Jedwali 7.1 Tathmini kiwango cha asifiksia.
DaliliHakuna asifiksiaAsifiksia ndogoAsifiksia kiasiAsifiksia kali
Mpigo wa moyoZaidi ya mipigo 100 kwa dakikaZaidi ya mipigo 100 kwa dakikaZaidi ya mipigo 60 kwa dakikaChini ya mipigo 60 kwa dakika
Rangi ya ngoziWaridiBuluu kidogoBuluu wastaniBuluu sana
Mkondo wa kupumuaKuliaKuliaKupumua lakini sio sanaKutopumua wala kutweta
Kusonga kwa miguu na mikonoInasonga vizuriKusonga kidhaifuKutosongaKutosonga
Kuchafuliwa na mekoniamuLaLaLabdaKawaida
UhaishajiHakuna hajaMwitiko wa harakaMwitiko mzuriAnachukua muda mrefu kuitika

Tathmini kiwango cha asifiksia chini ya sekunde 5. Fanya hivyo haraka lakini usiwe na hofu.

Lazima utoe huduma ya kumhaisha mtoto katika muda wa dakika moja baada ya kuzaliwa. Kwa hivyo, ni rahisi kukadiria mpigo wa moyo kuliko kuhesabu. Ni rahisi na haraka kutazama mkondo wa pumzi zake kuliko kuhesabu kiwango cha pumzi. Jedwali 7.2 linaorodhesha dalili zinazoonyesha kilicho na kisicho cha kawaida baada ya kuzaliwa.

Jedwali 7.2 Ugunduzi wa kawaida na usio wa kawaida kwa mtoto mchanga mara tu baada ya kuzaliwa.
IsharaUgunduzi wa kawaidaUgunduzi usio wa kawaida
RangiYafaa kuwa waridi

Buluu au yenye sinosisi (ukosefu wa oksijeni ya kutosha)

Nyeupe, (weupe) anemia

Umanjano

PumziPumzi 40-60 kwa dakika

Hakuna pumzi

Kiwango cha kupumua ni chini ya 30 kwa dakika

Mitweto (pumzi chache mno na zenye ugumu)

Kiwango cha mpigo wa moyoMipigo 120-160 kwa dakika

Hakuna mpigo wa moyo

Mpigo wa moyo ni chini ya 100 kwa dakika

 
Siha ya misuliMikono na miguu ya mtoto aliyezaliwa baada ya kutimiza umri kamili wa ujauzito imeyojikunja kidogoKujikunja duni kwa miguu na mikono, dhaifu (Picha 7.2), inayoashiria asifiksia kali inayoathiri ubongo
MatendohiariMtoto huhisi na kuitika kidole kinapowekwa kwenye kaakaa la kinywa chakeMtoto hahisi wala kuitika unapoligusa kaakaa la kinywa chake.

“Chini ya” inaweza kubadilishwa na alama , kwa mfano > 30 kwa dakika.

7.2.2 Kabla ya uhaishaji

7.4 Utaratibu wa uhaishaji wa mtoto mchanga