7.4.1 Sekunde tano za kwanza
Jedwali 7.3 linatoa muhtasari wa mambo utakayofanya ukiona dalili za asifiksia katika sekunde 5 za kwanza baada ya mtoto kuzaliwa. Habari zaidi zimetolewa baada ya maelezo haya ya jumla.
Mtoto mchanga anafanya nini | Tathmini | Kitendo |
---|---|---|
Analia na kusongesha miguu na mikono | Labda mtoto ni mwenye afya | Uhaishaji hauhitajiki |
Anapumua kidhaifu, hasongeshi mikono wala miguu, ana sinosisi kiasi | Labda ana asifiksia kiasi | Pitisha hewa safi ukisita Kadiria kiwango cha mpigo wa moyo |
Halii, hapumui, hatweti wala kusongesha mikono na miguu. Mikono na miguu ni dhaifu. Ana sinosisi au mwili wake una mekoniamu | Labda asifiksia kali | Ita msaidizi (jamaa au mtu mwingine). Tumia sirinji ya balbu. Fyonza kwenye kinywa, pua na maeneo ya koromeo chini ya sekunde 5. Pitisha hewa ukisita |
Halii, hapumui, hatweti wala kusongesha mikono na miguu. Mikono na miguu ni dhaifu. Ana sinosisi au mwili wake una mekoniamu | Kiwango cha mpigo moyo ni zaidi ya 60 kwa dakika | |
Halii, hapumui, hatweti wala kusongesha mikono na miguu. Mikono na miguu ni dhaifu. Ana sinosisi au mwili wake una mekoniamu | Kiwango cha mpigo moyo ni chini ya 60 kwa dakika | Tekeleza vitendo vyote vilivyo kwenye jedwali hili na pia uusinge moyo (Picha 7.4). |
7.4 Utaratibu wa uhaishaji wa mtoto mchanga