7.4.1 Sekunde tano za kwanza

Jedwali 7.3 linatoa muhtasari wa mambo utakayofanya ukiona dalili za asifiksia katika sekunde 5 za kwanza baada ya mtoto kuzaliwa. Habari zaidi zimetolewa baada ya maelezo haya ya jumla.

Jedwali 7.3 Vitendo kama mwitiko kwa dalili za asifiksia ya mtoto mchanga
Mtoto mchanga anafanya niniTathminiKitendo
Analia na kusongesha miguu na mikono Labda mtoto ni mwenye afyaUhaishaji hauhitajiki
Anapumua kidhaifu, hasongeshi mikono wala miguu, ana sinosisi kiasiLabda ana asifiksia kiasi

Pitisha hewa safi ukisita

Kadiria kiwango cha mpigo wa moyo

Halii, hapumui, hatweti wala kusongesha mikono na miguu. Mikono na miguu ni dhaifu. Ana sinosisi au mwili wake una mekoniamuLabda asifiksia kali

Ita msaidizi (jamaa au mtu mwingine).

Tumia sirinji ya balbu. Fyonza kwenye kinywa, pua na maeneo ya koromeo chini ya sekunde 5.

Pitisha hewa ukisita

Halii, hapumui, hatweti wala kusongesha mikono na miguu. Mikono na miguu ni dhaifu. Ana sinosisi au mwili wake una mekoniamuKiwango cha mpigo moyo ni zaidi ya 60 kwa dakika
Halii, hapumui, hatweti wala kusongesha mikono na miguu. Mikono na miguu ni dhaifu. Ana sinosisi au mwili wake una mekoniamu Kiwango cha mpigo moyo ni chini ya 60 kwa dakikaTekeleza vitendo vyote vilivyo kwenye jedwali hili na pia uusinge moyo (Picha 7.4).

7.4 Utaratibu wa uhaishaji wa mtoto mchanga

7.4.2 Chunguza kiwango cha mpigo wa moyo wa mtoto mchanga