7.4.6 Mguse kwa upole ili kumchochea kuanza upumuaji au kumsaidia katika kupumua

Mchoro 7.10 Mpe mguso chochelezi kwa upole. Sugua fumbatio la mtoto ukienda juu na chini. Papasa upande wa chini wa nyayo kwa vidole vyako.

Usimchochee kwa vitendo hivi.

Aina hizi za kuchochea ni hatari na zinaweza kumjeruhi mtoto huyu mchanga.

  • Usimpige kofi mgongoni.
  • Usimminye ngome ya mbavu.
  • Usisukume mapaja ya mtoto kwenye fumbatio lake.
  • Usitanue msuli (sfinkta) wa mkundu.
  • Usitumie vishinikizo moto au baridi wala kumwogesha kwa maji moto au baridi.
  • Usitingize kiungamwana.

7.4.5 Ondoa vizuizi kwenye kinywa na pua

7.4.7 Iwapo utatambua asifiksia, anza uhaishaji!