7.4.7 Iwapo utatambua asifiksia, anza uhaishaji!

Mlalishe chali mtoto huyu mchanga huku shingo lake likiwa limenyooshwa kidogo jinsi ilivyoonyeshwa kwenye picha ya kwanza katika mchoro 7.11. Fyonza kinywa na pua kwa sirinji aina ya balbu. Kufyonza hufungua njia ya hewa (Picha 7.9).

Mchoro 7.11 Weka kichwa katika nafasi ambapo njia yake ya hewa itakuwa wazi: Mchor wa kwanza ni sahihi. Kidevu kimegeuzwa kiasi kifaacho. Katika mchoro wa katikati, kichwa kimeinamishwa nyuma sana. Shinikizo linabana umio wa pumzi (trakea) shingoni mwake. Katika mchoro wa mwisho, kichwa hakijainamishwa vya kutosha. Kidevu kimekaribia kifua sana na njia ya hewa imebanwa.
  • Simama upande wa kichwa cha mtoto (Mchoro 7.12).
Mchoro 7.12 Nafasi mwafaka ya kumweka mtoto mchanga unapotumia mfuko wa ambu.

Ikiwa mpigo wa moyo wa apeksi ni zaidi ya mipigo 60 kwa dakika:

  • Pitisha hewa kwa barakoa yenye ukubwa ufaao na mfuko wa ambu unaopitisha hewa wenyewe. Barakoa inafaa kutosha jinsi ilivyoonyeshwa katika Mchoro 7.13. Tengeneza kizibo imara kati ya barakoa na uso wa mtoto ili hewa isipite kutoka kwa barakoa hiyo. Usilazimishe barakoa kwenye uso wa mtoto, kwani unaweza kusukuma kidevu kuelekea kwenye kifua cha mtoto na uishie kubana njia yake ya hewa. (Mchoro wa tatu katika Mchoro 7.11.)

Ikiwa mpigo wa moyo wa apeksi ni chini ya mipigo 60 kwa dakika:

  • Usinge moyo (Mchoro 7.4) na upitishe hewa safi kwa kusita kwa mfuko wa ambu.
Mchoro 7.13 Ukubwa unaofaa na usiofaa wa barakoa: Mchoro ulio upande wa juu ni sahihi: barakoa inafunika kinywa, pua na kidevu. Mchoro ulio chini upande wa kushoto si sahihi: barakoa ni kubwa sana na inafunika macho huku ikiendelea na kufunika kidevu pia. Mchoro ulio chini upande wa kulia si sahihi: barakoa ni ndogo sana na haifuniki pua wala mdomo.

7.4.6 Mguse kwa upole ili kumchochea kuanza upumuaji au kumsaidia katika kupumua

7.4.8 Pitisha hewa safi kwa kiasi cha pumzi 40 kwa dakika