7.5 Utunzaji muhimu wa mara moja wa mtoto mchanga

Sehemu ya mwisho ya Kipindi hiki cha somo inakukumbusha kuhusu utunzaji muhimu wa mtoto mchanga. Toa utunzaji huu kwa watoto wote pasipo kujali iwapo wana dalili za asifiksia. Kiungamwana kinapokatwa, mabadiliko mengi ya kifisiolojia mwilini mwa mtoto humsaidia kuzoea maisha ya nje ya mwili wa mama yake. Ni vigumu sana kumudu nje kuliko ndani ya uterasi ambapo ni salama. Toa utunzaji wa kimsingi kwa mtoto mchanga ili kumsaidia kujikinga dhidi ya hatari za kiafya zilizoorodheshwa katika Kisanduku 7.1.

Kisanduku 7.1 Hatari za Kiafya kwa watoto wachanga

Watoto wachanga huhitaji utunzaji ili kuzuia matatizo haya:

  • Damu kutoka yenyewe kwenye ufereji wa utumbo kutokana na ukosefu wa vitamini K
  • Kutokwa na damu kutokana na majeraha yanayotokana na uzazi (hujitokeza baadaye zaidi baada ya kuzaa ambapo skalpu hufura na kuhitaji rufaa ya haraka)
  • Maambukizi ya macho kutokana na Klamidia trakomati na Kisonono cha Neiseria. (Bakteria hizi ni visababishi vikuu vya maambukizi ya zinaa. Mtoto anaweza kupata maambukizi haya anapopita kwenye njia ya uzazi.)
  • Baadhi ya magonjwa yanayozuilika kwa chanjo kama polio na kifua kikuu.
  • Hipothemia (kuwa baridi sana)
  • Hipoglisimia (kiwango cha chini cha glukosi kwenye damu)
  • Maambukizi ya VVU kutoka kwa mama hadi kwa mtoto iwapo mama ana VVU.

Magonjwa yanayozuilika kwa chanjo yamejadiliwa kwa kina katika Moduli ya Magonjwa ya kuambukiza, Vikao vya 3 na 4 vya Somo.

Uzuiaji wa maambukizi ya VVU kutoka kwa mama hadi kwa mtoto umeelezewa katika Moduli ya Utunzaji katika ujauzito, Kipindi cha 17 cha Somo. Dawa na utaratibu wa uzuiaji wa maambukizi ya VVU kutoka kwa mama hadi kwa mtoto umeelezewa katika Moduli ya Magonjwa ya kuambukiza, Kipindi cha 27 cha Somo.

Kwa kuzingatia hatari za kiafya zilizo kwenye Kisanduku 7.1, wape watoto wote utunzaji huu muhimu:

  • Funga kiungamwana upana wa vidole viwili kutoka kwa fumbatio la mtoto. Funga maara ya pili upana wa vidole viwili kutoka kwa kifungo cha kwanza. Kata kiungamwana katikati ya kifungo cha kwanza na cha pili. Hakikisha kuwa shina la kiungamwana halitoki damu na si fupi sana.
  • Weka lihamu ya tetrasiklini kwenye macho mara moja tu. Lihamu hii hukinga dhidi ya maambukizi ya macho.
  • Dunga sindano iliyo na miligramu 1 ya vitamini K kwenye msuli upande wa mbele katikati mwa paja. Vitamini K huzuia damu kutoka yenyewe.
  • Mpe kipimo cha kwanza ya chanjo ya polio kwa kinywa na dawa ya chanjo dhidi ya kifua kikuu (BCG).
  • Mweke mtoto kwenye fumbatio la mama katika hali ya mgusano wa ngozi kwa ngozi na mama. Wafunike kwa blanketi na uweke kofia au shali yenye joto kwenye kichwa cha mtoto. Ni lazima kiwango cha joto cha mtoto kisalie zaidi ya sentigredi 36.
  • Hakikisha kuwa mtoto ananyonya vizuri na mama anatoa maziwa ya kutosha. Iwapo maziwa ya mama hayapendelewi, hakikisha kuwa chakula mbadala cha kutosha kipo. Anzisha unyonyeshaji mapema bila kumpa chakula kingine chochote ila kuna sababu mwafaka za kutonyonyesha. Kwa mfano, mama aliye na VVU hawezi kunyonyesha.
  • Iwapo mama ana VVU, mpe mtoto matibabu ya kumkinga dhidi ya VVU.

Ratiba ya uchanjaji ya chanjo zote zilizo kwenye Moduli ya Uchanjaji.

Utajifunza yote kuhusu unyonyeshaji katika Moduli yaUtunzaji baada ya kuzaa. Unyonyeshaji na VVU vimeelezewa katika Moduli ya Magonjwa ya kuambukiza, Kipindi cha 27 cha Somo.

7.4.9 Chunguza motto huku ukumpitishia hewa

Muhtasari wa Kipindi cha 7