8.8 Utunzaji wa wanawake walio na milalo mibaya ya watoto au mimba ya zaidi ya mtoto mmoja

Jinsi ulivyoona katika Kipindi hiki, mlalo wowote isipokuwa ule wa kutanguliza veteksi unazo hatari zake kwa mama na mtoto. Kwa sababu hii, wanawake wote wanaokumbwa na milalo isiyo ya kawaida au mimba ya zaidi ya mtoto mmoja wanafaa kupata huduma bora kutoka kwa wataalam wakuu wa afya. Wanawake hawa wanapaswa kuhudumiwa katika kituo cha afya kilicho na uwezo wa kutoa huduma bora ya dharura ya uzazi. Utambuzi wa mapema na rufaa kwa mwanamke aliye na mojawapo ya hali hizi inaweza kuokoa maisha yake pamoja na ya mtoto wake.

  • Je, ni nini unachoweza kufanya ili kupunguza hatari zinazotokana na mlalo mbaya wa fetasi au mimba ya zaidi ya mtoto mmoja kwa wanawake unaowatunza?

  • Katika utunzaji maalum wa manawake katika ujauzito, chunguza mlalo usio wa kawaida wa fetasi kila wanapokutembelea baada ya majuma 36 ya ujauzito. Ukigundua mlalo usio wa kawaida au mimba ya zaidi ya mtoto mmoja, mpe mwanamke huyo rufaa kabla ya leba kuanza.

    Mwisho wa jibu

8.7.3 Athari za mimba ya pacha

Muhtasari wa Kipindi cha 8