Malengo ya Somo la Kipindi cha 8

Baada ya Kipindi hiki cha somo utaweza:

8.1 Kufafanua na kutumia kwa usahihi maneno yote muhimu yaliyoandika kwa herufi nzito. (Maswali ya kujitathmini 8.1 na 8.2)

8.2 Kueleza jinsi ya kutambua fetasi iliyotanguliza veteksi. Tambua veteksi kwenye fetasi iliyo katika mlalo mbaya na isiyokuwa katika nafasi ya kawaida. (Maswali ya kujitathmini 8.1 na 8.2)

8.3 Kueleza visababishi na matatizo ya fetasi na mama kutokana na mlalo mbaya wa fetasi katika leba ya mimba iliyokomaa. (Swali la kujitathmini 8.3)

8.4 Kuelezea jinsi ya kutambua mimba ya zaidi ya mtoto mmoja na matatizo yanayoweza kutokea. (Swali la kujitathmini 8.4)

8.5 Kueleza lini na jinsi ya kumpa rufaa mwanamke mwenye leba kutokana na mlalo usio wa kawaida wa fetasi au mimba ya zaidi ya mtoto mmoja. (Swali la kujitathmini 8.4)

Kipindi cha 8 cha Somo Milalo Isiyo ya kawaida na mimba ya zaidi ya mtoto mmoja

8.1 Milalo ya kawaida na isiyo ya kawaida