8.1 Milalo ya kawaida na isiyo ya kawaida

8.1.1 Mlalo wa kutanguliza veteksi

Katika takriban asilimia 95 ya uzazi, sehemu ya fetasi inayotangulia ukingoni mwa pelvisi ni sehemu iliyo juu zaidi ya kichwa cha fetasi. Sehemu hii ya kichwa huitwa veteksi (Picha 8.1). Hali hii huitwa mlalo wa kutanguliza veteksi. Tambua kuwa kidevu cha mtoto kimepindwa kuelekea kwenye kifua chake. Veteksi ndiyo sehemu inayotangulia kuingia kwenye pelvisi ya mama. Katika nafasi na hali hii, kichwa cha mtoto husemekana kuwa “kimejikunja vizuri”.

Picha 8.1 Mtoto aliyejikunja vizuri katika mlalo wa kutanguliza veteksi kabla ya kuzaliwa, kuhusiana na pelvisi ya mama. (Imetolewa: Shirika la Afya Duniani, Kudhibiti Matatizo katika Ujauzito na Kuzaa.)

Mwanzoni mwa ujauzito, mtoto hugeuzwa upande mwingine. Upande wa chini wa mtoto huelekezwa chini kuelekea seviksi ya mama. Mlalo huu huitwa wa kutanguliza matako. Mwanzoni mwa kukua, kichwa cha fetasi huwa kikubwa kuliko matako yake. Mara nyingi kichwa huchukua kaviti pana zaidi, yaani fandasi ya uterasi. Fetasi inapoendelea kuwa kubwa, matako huwa makubwa kuliko kichwa. Mtoto hugeuza mlalo wake mwenyewe ambapo matako yake sasa huchukua fandasi. Kwa ufupi, mwanzoni mwa ujauzito fetasi nyingi huwa katika mlalo wa kutanguliza matako. Baadaye katika ujauzito, fetasi nyingi hujipindua na kutanguliza veteksi.

Malengo ya Somo la Kipindi cha 8

8.1.2 Milalo mibaya