8.2 Visababishi na athari za milalo mibaya na hali ya kutokuwa katika nafasi ya kawaida 

Unaweza kukosa kutambua ni kwa nini mtoto yuko katika mlalo usio wa kawaida au katika nafasi isiyo ya kawaida wakati wa kuzaa. Hata hivyo, hali hizihuongeza hatari ya mlalo mbaya na kutokuwa katika nafasi ya kawaida:

Mimba ya zaidi ya mtoto mmoja ndio mahusiko ya sehemu ya 8.7 ya Kipindi hiki. Ulijifunza kuhusu plasenta privia katika Moduli ya Utunzaji katika Ujauzito, Kipindi cha 21.

  • Kiowevu cha amnioni kingi au kidogo zaidi.
  • Tyuma kwenye uterasi inayozuia fetasi kupinduka kutoka katika mlalo wa kutanguliza matako hadi ule wa kutanguliza veteksi katika siku za mwisho wa ujauzito. (Tyuma ni tishu inayokua katika hali isiyo ya kawaida.)
  • Umbo lisilo la kawaida la pelvisi.
  • Rusu za misuli zilizolegea kwenye kuta za uterasi.
  • Mimba ya zaidi ya mtoto mmoja.
  • Plasenta privia (plasenta iliyofunika mwanya wa seviksi kabisa au kwa kiasi).

Iwapo mtoto anajitokeza katika mlalo au nafasi isiyo ya kawaida, inaweza kuwa vigumu kukamilisha miendo saba mikuu. Ulijifunza kuhusu miendo hii katika Vipindi vya 3 na 5. Hatimaye, uzazi huwa mgumu zaidi na hatari ya matatizo haya huongezeka.

Ulijifunza kuhusu kupasuka kwa membrani kabla ya muda wake katika Kipindi cha 17 cha Moduli ya Utunzaji katika Ujauzito, sehemu ya 2.

  • Kupasuka kwa membrani za fetasi kabla muda wake.
  • Leba kabla ya muda wake.
  • Mikazo ya polepole, isiyotabirika na unaodumu kwa muda mfupi.
  • Mikazo isiyopatana na yenye uchungu zaidi, na leba kuendelea pole pole au kutoendelea kabisa.
  • Leba iliyokaa kwa muda mrefu na iliyozuiliwa, inayoweza kusababisha kupasuka kwa uterasi (Vipindi vya 9 na 10).
  • Kutokwa na damu baada ya kuzaa (Kipindi cha 11) .
  • Kuathirika kwa fetasi na mama kunakoweza kusababisha kifo cha mtoto na/au mama.

Kumbuka matatizo haya unapojifunza kuhusu aina zinazotokea mara nyingi za mlalo mbaya na jinsi ya kuzitambua.

8.1.3 Kutokuwa katika nafasi ya kawaida

8.3 Mlalo wa kutanguliza matako