8.3 Mlalo wa kutanguliza matako

Katika mlalo wa kutanguliza matako, fetasi hujilaza matako yake yakiwa nyuma. Matako na/au miguu ndizo sehemu zinazotangulia wakati wa kuzaliwa. Mlalo wa kutanguliza matako hutokea katika takriban asilimia 3-4 za uzazi unaotendeka baada ya wiki 34 ya ujauzito.

  • Je, ni lini ambapo mlalo wa kutanguliza matako huwa nafasi ya kawaida kwa fetasi?

  • Mwanzoni mwa ujauzito, matako ya mtoto huelekezwa chini kuelekea kwenye seviksi ya mama. Kichwa ndicho sehemu kubwa zaida katika awamu hii ya ukuaji. Kichwa chake huwa kwenye fandasi ya uterasi, ambayo ndiyo sehemu pana zaidi ya kaviti ya uterasi.

    Mwisho wa jibu

8.2 Visababishi na athari za milalo mibaya na hali ya kutokuwa katika nafasi ya kawaida 

8.3.1 Visababishi vya mlalo wa kutanguliza matako