8.3.1 Visababishi vya mlalo wa kutanguliza matako

Unaweza kuona kulala kingamo katika Picha 8.7 baadaye katika Kipindi hiki.

Katika hali nyingi, huoni sababu dhahiri inayoweza kuifanya fetasi kutanguliza matako baada ya muda kamili wa ujauzito. Mara nyingi mlalo wa kutanguliza matako wakati wa kuzaa huhusishwa na fetasi kulala kingamo mwanzoni mwa ujauzito. Kulala kingamo humaanisha kuwa fetasi imelala kwa upande kutoka upande mmoja hadi mwingine wa fumbatio ya mama, na imeangalia plasenta iliyojipandikiza kwa upande. Plasenta ikiwa mbele ya uso wa mtoto, inaweza kuzuia mchakato wa kawaida wa kupinduka. Wakati wa kupinduka mtoto hugeuza kichwa chini anapoendelea kuwa mkubwa katika ujauzito. Kutokana na haya, mtoto hugeuka kwa upande huo mwingine na kuishia katika mlalo wa kutanguliza matako. Mlalo wa kutanguliza matako katika leba unaweza pia kusababishwa na mambo haya:

  • Leba ya kabla ya muda wake ambayo huanza kabla ya mtoto kujipindua kutoka mlalo wa kutanguliza matako hadi ule wa kutanguliza veteksi.
  • Mimba ya zaidi ya mtoto mmoja, inaweza kuzuia kupinduka kikawaida kwa mtoto mmoja au wote wawili.
  • Polihadromino: kiasi kingi cha kiowevu cha amnioni. Kichwa cha fetasi hakiwezi kukabiliana na seviksi ya mama.
  • Hidrosefalasi “maji kwenye ubongo”. Kichwa cha fetasi ni kikubwa kupita kiasi kutokana na kuongezeka kupita kiasi kwa kiowevu kwenye ubongo.
  • Plasenta privia.
  • Kuzaa mtoto aliyekuwa katika mlalo wa kutanguliza matako katika mimba ya hapo awali.
  • Uterasi isiyojengeka kikawaida.

8.3 Mlalo wa kutanguliza matako

8.3.2 Utambuzi wa mlalo wa kutanguliza matako