8.3.4 Hatari za mlalo wa kutanguliza matako

Wape rufaa wote walio na hali ambazo mtoto ametanguliza matako waende katika kituo cha afya cha ngazi ya juu kilicho karibu.

Aina zote za mlalo wa kutanguliza matako husababisha hatari kuu kwa mtoto:

  • Kichwa cha fetasi hukwama kabla ya kuzaliwa.
  • Leba huzuiliwa fetasi iwapo kubwa kutolingana na ukubwa wa pelvisi ya mama.
  • Prolapsi ya kiungamwana (kuchomoza kwa kiungamwana) inaweza kutokea. Kiungamwana kinasukumwa nje kabla ya mtoto na kinaweza kubaniwa kwenye ukuta wa sevikisi au uke.
  • Plasenta inaweza kutenganishwa kutoka mahali pa plasenta kabla ya muda wake. (Huitwa kuchubuka kwa plasenta.)
  • Mtoto kujeruhiwa anapozaliwa. Kwa mfano kuvunjika mikono au miguu, kuharibika kwa neva, kuumia kwa ogani za ndani na uti wa mgongo.

Uzazi wa mlalo wa kutanguliza matako unaweza kusababisha kujeruhiwa kwa njia ya uzazi ya mama au jenitalia za nje zinaweza kutanuliwa kupita kiasi kwa sababu sehemu za fetasi haziwezi kupita.

Prolapsi ya kiungamwana katika mlalo wa kawaida wa kutanguliza veteksi ilielezewa katika Kipindi cha 17 cha Somo cha Moduli ya Utunzaji katika Ujauzito. Kuchubuka kwa Plasenta kulielezewa katika Kipindi cha 21 cha Somo.

  • Je, kuna athari gani kwa mtoto akikwama, leba imezuiliwa, kiungamwana kimechomoza au kukitokea kuchubuka kwa plasenta?

  • Matokeo ni haipoksia. Mtoto huyo hukoseshwa oksijeni na anaweza kukumbwa na kuharibika kwa ubongo kwa kudumu au afariki.

    Ulijifunza kuhusu visababishi na matokeo ya haipoksia katika Moduli ya utunzaji katika ujauzito.

    Mwisho wa jibu

8.3.3 Aina za mlalo wa kutanguliza matako

8.4 Mlalo wa kutanguliza uso