8.4 Mlalo wa kutanguliza uso

Mlalo wa kutanguliza uso hutokea wakati shingo la mtoto limerefushwa (limekunjwa kuelekea nyuma) kiasi kwamba kisogo kinagusa uti wa mgongo wa mtoto huyo (Picha 8.5). Katika hali hii, uso wa mtoto ndio unaotangulia.

Picha 8.5 Mlalo wa kutanguliza uso. (a) Kidevu cha mtoto kimeangalia upande wa mbele wa pelvisi. (b) Kidevu kimeangalia upande wa uti wa mgongo wa mama (Imetolewa: Shirika la Afya Duniani, jinsi ilivyo katika Picha 8.1).

Mpe mama rufaa iwapo mtoto aliye katika mlalo wa kutanguliza uso huku kidevu chake kikiwa kimeangalia upande wa uti wa mgongo wa mama hatazunguka na hivyo basi leba kuendelea kwa muda mrefu.

Takribani mimba ya 1 kwa kila 500 inayotimiza muda kamili huwa katika mlalo wa kutanguliza uso. Picha 8.5 yaonyesha jinsi kichwa kilivyojikunja shingoni. Watoto wanaojitokeza katika hali ambapo kidevu kimeangalia upande wa uti wa mgongo wa mama (Picha 8.5b) kwa kawaida huzunguka wenyewe katika leba. Wanajiweka katika hali ya “kidevu mbele”, ambayo hurahisisha kuzaliwa kwao. Hata hivyo wasipozunguka na kujiweka katika hali ya kidevu upande wa mbele wa pelvisi, huenda wasizaliwe kupitia ukeni. Kidevu cha mtoto hukwama kwenye sakramu ya mama. (Sakramu ni mfupa uliobinuka nyuma ya pelvisi.) Mtoto aliye katika hali hii lazima azaliwe kupitia upasuaji.

8.3.4 Hatari za mlalo wa kutanguliza matako

8.4.1 Visababishi vya mlalo wa kutanguliza uso