8.5.2 Utambuzi wa mlalo wa kutanguliza paji la uso

Mlalo wa kutanguliza paji la uso kwa kawaida haugunduliwi kabla ya mwanzo wa leba. Hata hivyo, wahudumu wa uzazi wenye uzoefu mwingi wanaweza kugundua mlalo wa kutanguliza paji la uso. Wakati wa uchunguzi wa fumbatio, kichwa huwa juu katika fumbatio la mama. Kichwa huonekana kikubwa mno na hakiteremki kuingia kwenye pelvisi, hata kukiwa na mikazo bora ya uterasi. Wakati wa kufanya uchunguzi ukeni, sehemu inayotangulia huwa juu na inaweza kuwa vigumu kuifikia. Unaweza kugusa mwanzo wa pua na macho. Lakini hauwezi kugusa kinywa, mwisho wa pua au kidevu. Pia unaweza kugusa fontaneli (utosi) ya mbele. Hata hivyo, baada ya saa fulani za kuwepo kwa leba, uvimbe mkubwa upande wa mbele ya fuvu la kichwa cha fetasi unaweza kuifunika alama hii.

Kumbuka wajihi wa uvimbe wa kawaida na fontaneli ya nyuma iliyoonyeshwa katika Picha 4.4.

8.5.1 Vinavyoweza kusababisha mlalo wa kutanguliza paji la uso

8.5.3 Matatizo ya mlalo wa kutanguliza paji la uso