8.6 Mlalo wa kutanguliza bega

Mlalo wa kutanguliza bega hautokei sana katika mimba iliyokomaa. Hata hivyo, mlalo wa kutanguliza bega hutokea iwapo fetasi imelala kingamano kwenye uterasi (Picha 8.7). Pengine haikukamilisha mvunguko ilipokuwa ikipinduka kutoka katika hali ya kutanguliza matako hadi kutanguliza veteksi. Labda imelala kingamano tangu mwanzoni mwa mimba. Mtoto akilala chali, huenda mgongo wake ndio kitangulizi. Iwapo mtoto amelala kifudifudi (ameangalia chini), mkono wake unaweza kujitokeza kupitia kwenye seviksi. Mtoto aliye katika hali ya kingamano hawezi kuzaliwa kupitia ukeni na leba hiyo huzuiliwa. Wape rufaa kwa haraka wenye watoto walio katika mlalo wa kutanguliza bega.

Usijaribu kumgeuza mtoto aliyeulalia upande wake.Isipokuwa mhudumu wa afya mwenye ujuzi amgeuze, mtoto huyo anafaa kuzaliwa kwa njia ya upasuaji.

Picha 8.7 Kujilaza kingamo (mlalo wa kutanguliza bega). Mtoto huyu hawezi kuteremka kwenye njia ya uzazi.

8.5.3 Matatizo ya mlalo wa kutanguliza paji la uso

8.6.1 Visababishi vya mlalo wa kutanguliza bega