8.6.1 Visababishi vya mlalo wa kutanguliza bega

Mlalo wa kutanguliza bega unaweza kusababishwa na vipengele vinavyohusu mama au fetasi.

Vipengele vinavyomhusu mama ni:

  • Ulegevu (udhaifu) wa misuli ya fumbatio na uterasi: hasa baada ya mimba kadhaa za hapo awali.
  • Matatizo kwenye uterasi.
  • Pelvisi iliyokaza (nyembamba kupindukia).

Vipengele vinavyoihusu fetasi ni:

  • Leba kabla ya muda kamili wa mimba kutimia
  • Mimba ya zaidi ya mtoto mmoja
  • Polihadromino
  • Plasenta privia
  • Je, “plasenta privia” na “polihadromino” huashiria nini?

  • Plasenta privia ni hali ya plasenta imeufunika mwanya wa seviksi kikamilifu au kwa kiasi. Polihadromino ni kiasi kingi cha kiowevu cha amnioni. Matatizo haya yote mawili yanaweza kusababisha milalo mibaya.

    Mwisho wa jibu

8.6 Mlalo wa kutanguliza bega

8.6.2 Utambuzi wa mlalo wa kutanguliza bega