8.6.2 Utambuzi wa mlalo wa kutanguliza bega

Unapotomasa fumbatio uterasi huonekana kuwa pana na urefu wa fandasi ni mdogo kuliko inavyotarajiwa kwa kipindi hiki cha ujauzito. Urefu ni mdogo kwa sababu kichwa wala matako ya mtoto hayako kwenye fandasi. Kwa kawaida unaweza kuhisi kichwa kwenye upande mmoja wa fumbatio la mama. Wakati wa uchunguzi wa ukeni, huenda usihisi kitangulizi mwanzoni mwa leba. Lakini leba ikiendelea vizuri, unaweza kuhisi mbavu za mtoto. Bega linapoingia ukingoni mwa pelvisi, mkono wa mtoto unaweza kuchomoza na kuonekana nje ya uke.

8.6.1 Visababishi vya mlalo wa kutanguliza bega

8.6.3 Matatizo ya mlalo wa kutanguliza bega