8.6.3 Matatizo ya mlalo wa kutanguliza bega

Matatizo ni haya:

  • Prolapsi (kuchomoza) ya kiungamwana
  • Kuathirika kwa mkono uliochomoza
  • Leba iliozuiliwa na uterasi iliyopasuka
  • Haipoksia ya fetasi na kifo

Kumbuka kuwa mlalo wa kutanguliza bega una maana kuwa mtoto hawezi kuzaliwa kupitia ukeni. Ukigundua mlalo wa kutanguliza bega kwa mwanamke aliye tayari katika leba, mpe rufaa mara moja aende katika kituo cha afya cha kiwango cha juu.

Katika visa vyote vya mlalo mbaya au kutokuwa katika nafasi ya kawaida, usijaribu kumgeuza mtoto kwa kutumia mikono yako! Ni daktari au mkunga maalum aliyehitimu tu anayepaswa kujaribu kumgeuza mtoto. Mpe mama rufaa ili yeye pamoja na mtoto wake waweze kupata huduma ya dharura ya uzazi.

8.6.2 Utambuzi wa mlalo wa kutanguliza bega

8.7 Mimba ya zaidi ya mtoto mmoja