8.7 Mimba ya zaidi ya mtoto mmoja

Sehemu hii inaeleza kuhusu mimba ya zaidi ya mtoto mmoja, ambayo ni zaidi ya fetasi moja kwenye uterasi. Zaidi ya asilimia 95 ya mimba ya zaidi ya mtoto mmoja ni pacha (fetasi mbili). Lakini unaweza pia kupata watatu (fetasi tatu), wanne (fetasi nne), watano (fetasi tano) na idadi zingine za juu. Uwezekano wa kupata zaidi ya fetasi moja hupunguka kulingana na ongezeko katika idadi ya fetasi. Visa vya kupata mapacha ni tofauti kwa kila nchi. Nchi zilizo Mashariki mwa Asia kama vile Japan na Uchina zina uwezekano mdogo wa visa vya upataji wa mapacha. Mashariki mwa Asia, 1 kati ya mimba 1000 ni pacha wa kidugu au pacha wasiofanana. Wafrika weusi wana uwezekano mkubwa wa kupata mapacha. Nchini Nigeria, 1 kati ya mimba 20 ni pacha wa kidugu. Mimba ya zaidi ya mtoto mmoja huhusishwa sana na upotezaji wa mimba katika awamu ya kwanza na watoto kufariki wakati wa kuzaliwa, hasa kutokana na kuzaliwa kabla ya muda kamili wa mimba kumalizika.

8.6.3 Matatizo ya mlalo wa kutanguliza bega

8.7.1 Aina za mimba ya pacha