8.7.1 Aina za mimba ya pacha

Mapacha wanaweza kufanana (wa monozaigoti) au wasifanane na wa kidugu (wa daizigoti). Mapacha wa monozaigoti hutokea kwenye yai moja lililotungishwa (zaigoti). Kwa hivyo wao huwa wa jinsia moja na hutumia plasenta moja. Kwa upande mwingine, mapacha wa daizigoti hutokana na zaigoti mbili tofauti. Kwa hivyo, wanaweza kuwa wa jinsia moja au la na pia wana plasenta tofauti. Picha 8.8 inaonyesha aina za mimba ya mapacha na mchakato wa kukua kwake.

Picha 8.8 Aina za mimba ya pacha: (a) Wa Kidugu au pacha wasiofanana ambao kila mmoja anayo plasenta yake. Hata hivyo, iwapo plasenta hizo zitakaribiana sana, zinaweza kuungana. (b) Pacha wanaofanana hutumia plasenta moja lakini kila mmoja anayo membreni yake ya fetasi.

8.7 Mimba ya zaidi ya mtoto mmoja

8.7.2 Utambuzi wa mimba ya pacha