8.7.2 Utambuzi wa mimba ya pacha

Wakati wa uchunguzi wa fumbatio, unaweza kutambua vitu hivi:

  • Uterasi ni kubwa zaidi ya inavyotarajiwa katika kipindi hicho mimba.
  • Uterasi inaonekana kuwa mviringo na pana na kusonga kwa fetasi kuonekana katika sehemu kubwa. (Muundo wa uterasi katika mimba iliyokoma wa mtoto mmoja aliye katika mlalo wa kutanguliza veteksi huonekana kuwa na umbo la moyo; kama mviringo upande wa juu na nyembamba upande wa chini).
  • Unaweza kuhisi vichwa viwili.
  • Midundo miwili ya moyo ya fetasi inaweza kusikika. Watu wawili wakisikiza kwa wakati mmoja na wasikie angalau midundo 10 tofauti, huenda kuna fetasi mbili (Picha 8.9).
  • Uchunguzi wa kutumia mawimbi sauti ya tiba unaweza kutoa utambuzi bora wa mimba ya pacha.
Picha 8.9 Watu wawili wanaweza kuwasikiza pacha, kwa kugonga kwa mwendo sawa na midundo ya mioyo ya hizo fetasi mbili.

8.7.1 Aina za mimba ya pacha

8.7.3 Athari za mimba ya pacha