8.7.3 Athari za mimba ya pacha

Wanawake walio na mimba ya pacha hutatizika sana na matatizo madogo madogo ya ujauzito kama vile kichefuchefu cha mjamzito asubuhi, kichefuchefu, na kiungulio. mimba ya pacha ni kisababishi kimoja cha hiparemisisi gravidaramu (kichefuchefu kingi na kutapika kupindukia katika ujauzito). Kina mama wa mapacha pia wamo katika hatari zaidi ya kupata anemia itokanayo na ukosefu wa ayoni na folati katika ujauzito.

  • Je, unaweza kupendekeza ni kwa nini anemia ni hatari kubwa katika mimba ya zaidi ya mtoto mmoja?

  • Lazima mama apate virutubishi vya kuwalisha watoto wawili (au zaidi). Ikiwa hapati ayoni na folati ya kutosha katika lishe yake au kupitia katika vyakula vya ziada, atapata anemia.

    Mwisho wa jibu

Matatizo mengine ni kama haya:

  • Matatizo ya hipatensheni yanayohusiana na ujauzito kama vile dalili zinazotangulia eklampsia (prekilampsia) na eclampsia (ugonjwa wa ujauzitoni) hutokea sana katika ujauzito.
  • Dalili za shinikizo zinaweza kutokea mwishoni mwa ujauzito kutokana na uzani na ukubwa ulioongezeka wa uterasi.
  • Leba kuanza yenyewe mapema na hatimaye kuzaa au membreni kupasuka kabla ya muda kamili wa ujauzito kutimia.
  • Ugumu katika kupumua (upungufu wa hewa kutokana na ukuaji wa haraka wa uterasi) ni tatizo jingine linalotokea sana.

Watoto pacha wanaweza kuwa wadogo ikilinganishwa na umri wa ujauzito huo. Watoto pacha wana uwezekano mkubwa wa kupata matatizo yanayohusiana na uzani wa chini wa kuzaliwa. (Matatizo haya ni kama kuwa wenye kuathiriwa na maambukizi kwa urahisi, kupoteza joto na ugumu katika kunyonya).

Utajifunza kwa kina kuhusu watoto waliozaliwa wakiwa na uzani wa chini katika moduli ya Utunzaji baada ya kuzaa.

  • Mlalo mbaya hutokea sana katika mimba ya pacha. Pia, wanaweza kufungamana shingoni mmoja akiwa katika mlalo wa kutanguliza veteksi huku mwingine akitanguliza matako. Hatari zilizoelezewa hapo awali zinazohusiana na milalo mibaya pia zinaweza kutokea: prolapsi (kuchomoza) ya kiungamwana, minyweo duni ya uterasi, leba iliyokaa sana au iliyozuiliwa, kutokwa na damu muda tu baada ya kuzaa, na haipoksia ya fetasi na kufa.
  • Kupata pacha walioungana (pacha muungano, walioungana kwenye kichwa, kifua, fumbatio au mgongo) pia kunawezekana, ingawa ni nadra.

8.7.2 Utambuzi wa mimba ya pacha

8.8 Utunzaji wa wanawake walio na milalo mibaya ya watoto au mimba ya zaidi ya mtoto mmoja