9.2.2 Kitangulizi kisicho cha kawaida na mimba nyingi

Mchoro 9.1 Kutolingana kwa kichwa na pelvisi: pelvisi ya mama huyu ni ndogo sana kwa kichwa cha mtoto wake.

Ukaaji wa kitangulizi au kukaa vibaya ni sababu zingine kuu za leba iliyozuiliwa.

  • Je, unaweza kutofautisha kati ya maneno haya mawili na kukumbuka baadhi ya vitangulizi vya fetasi visivyokuwa vya kawaida na kutokuwa katika mkao wa kawaida katika uterasi kutoka Kipindi cha 8 cha Somo?

  • Kitangulizi kisicho cha kawaida ni kitangulizi chochote bali sio kipeo, ambayo ni wakati fuvu la kichwa cha mtoto hutangulia kwanza. Kawaida vitangulizi visivyokuwa vya kawaida huwa makalio na bega itakapotoka “bega kwanza”. (Kitanguliza cha makalio ni wakati makalio ya mtoto na/au miguu hutoka kwanza.) Mkao mbaya in wakati mtoto huwa “kichwa chake kiko chini” (kichwa ndio–kitangulizi) lakini kipeo kiko pahali hapafai ikilinganishwa na pelvisi ya mama. Aina mbili za kawaida zaidi za mkao wa fetasi usiofaa husababisha utangulishi wa uso na paji la uso.

    Mwisho wa jibu

Pia ulijifunza kuhusu kupata mimba nyingi katika Kipindi cha 8 cha Somo. Leba inaweza kuzuiliwa na mapacha waliofungiana au mapacha walioshikana. Mapacha waliofungiana ni watoto wawili “waliofungana” pamoja kwa shingo wakati pacha wa kwanza akiwa katika kutanguliza tako na wa pili yuko katika kutanguliza kichwa mwanzo. Mapacha walioshikana huwa wameungana kwa kifua, kichwa, au eneo lingine lolote lile.

9.2.1 Kutolingana kwa kichwana pelvisi

9.2.3 Ulemavu wa fetasi