9.2.4 Njia ya uzazi isiyokuwa ya kawaida

Leba iliyozuiliwa inaweza kusababishwa na njia ya uzazi ya mama isiyokuwa ya kawaida. Mama anaweza kuwa na tyuma (ukuwaji au uvimbe wa tishu) katika kaviti ya pelvisi. Au mama anaweza kuwa na kovu katika njia ya uzazi sababu ya njia kali ya ukeketaji. Au anaweza kuwa na msamba ambayo imebana, usio panuka ili kupitisha mtoto. (Msamba ni ngozi iliyo katikati ya ufa wa uke na mkundu.)

Ukeketaji ndio lengo la Kipindi cha 5 Somo katika moduli ya Balehe na afya ya uzazi ya vijana.

9.2.3 Ulemavu wa fetasi

9.3 Dalili za leba iliyozuiliwa