9.3.2 Bandl’s ring

Bandl’s ring ni jina linalopewa mbonyeo katikati ya uterasi ya juu na chini, karibu na kitovu. Haufai kuona au kuhisi Bandl's ring ukipima fumbatio ya mama katika leba ya kawaida (Mchoro 9.2a). Unapoona au kuhisi Bandl's ring (Mchoro 9.2b), ni ishara ya mwisho ya leba iliyozuiliwa. Juu ya mbonyeo hiuu kuna sehemu ya juu ya uterasi ambayo ni nene mno. Sehemu hii ya juu imevutwa kwa upande wa juu (kurudi ndani) kuelekea kwenye mbavu za mama. Chini ya Bandi's ring ni uvimbe (uliofura), mkonde hatari, sehemu ya chini ya uterasi. Sehemu ya chini ya fumbatio inaweza zaidi kuvimbishwa na kibovu kilichojaa na gesi ndani ya matumbo.

Mchoro 9.2 (a) Umbo la kawaida la fumbatio iliyo na mimba wakati wa leba, kwa mwanamke aliye lala chali; (b) Bandi's ring kwa fumbatio ya mama aliye kwa leba iliyozuiliwa.

9.3.1 Utathmini wa dalili za kliniki ya hali iliyozuiliwa

9.3.3 Ushahidi kutoka kwa patografu