9.4 Udhibiti wa leba iliyozuiliwa

Iwapo rekondi ya utanuzi wa servikisi imefika mstari wa Tahadhari kwa patografu, jaribu kuondoa kizuizi kabla haijafikia mstari wa hatua. Ulijifunza taratibu hizi katika Moduli ya huduma za ujauzito (Kipindi cha 22 cha Somo) na ujuzi wako kwa mafunzo ya vitendo. Zimeelezewa hapa kwa ufupi:

  • Ikiwa mwanamke ana dalili za mshtuko, mpe kiowevu aina ya Normal Saline au Ringer’s Lactate ili kuregeshea kiowevu mwilini. (Dalili za mshtuko ni mpigo wa mshipa wa haraka na shinikizo la damu ilio chini.) Tumia kanula kubwa (Nambari. 18 au 20) Mpe lita 1 ya viowevu, haraka iwezekanavyo. Rudia lita 1 kila baada ya dakika 20 mpaka kiwango cha mpigo wa mshipa upungue chini ya 90 kwa kila dakika, na shinikizo la damu diastoli ifikie 90 mmHg au zaidi (Diastoli ya shinikizo la damu ni wakati roho inatulia baada ya piga.)
  • Kama unafikiri kizuizi ni kutokana na kibofu cha mkojo kilio jaa sana, toa na catheta. Safisha msamba na weka katheta kwa kibofu cha mama. Weka mkojo katika chombo kilicho funikwa. Kutoa kizuizi hiki inawezesha mtoto kuzaliwa. Kumbuka kwa kawaida ni vigumu sana kuweka katheta kwenye kibofu kwa mwanamke aliye na leba iliyozuiliwa. Urethra pia huwa imefungwa na kichwa cha mtoto, ambacho kiko ndani kabisa.

Mpeleke mama haraka kwa kituo cha afya ambapo huduma ya upasuaji inapatikana (Mchoro 9.4). Anaweza kuhitaji uzalishaji wa dharura kwa operesheni ya upasuaji ilikutoa mtoto akiwa hai na kuokoa maisha yake. (Operesheni ya siza ni wakati fumbatio yake na uterasi hufunguliwa kwa kukatwa ili kutoa mtoto.)

Mchoro 9.4 Usichelewe kurufaa mwanamke ambaye leba yake ina kizuizi.

9.3.3 Ushahidi kutoka kwa patografu

9.5 Matatizo yanayotokana na leba iliyozuiliwa