9.5.1 Fistula

Fistula ni ufunguzi usiokuwa wa kawaida (kwa kawaida hutokea kwa sababu ya tishu kukatika) kati ya:

  • Uke na kibofu cha mkojo
  • Uke na rektamu
  • Uke na urethra (neli ambayo huleta mkojo kutoka kwa kibofu hadi ufunguzikatika valva)
  • Uke na ureta(mshipa ambayo huleta mkojo kutoka kila figo kwa kibofu cha mkojo)
Mchoro 9.5 Fistula ni tatizo la leba iliyozuiliwa inayosababisha matatizo zaidi.

Fistula inapitisha mkojo au kinyesi ndani ya uke na kisha hutokea kwa njia isiyozuilika. Mwanamke aliye na fistula anaweza kutoa mkojo au kinyesi wakati anapotembea au kufanya shughuli yoyote ya kila siku. Uchafu huu uchafua nguo zake na huleta harufu mbaya (Mchoro 9.5). Kwa sababu ya athari hizi, mume wake na familia wanaweza kumshutumu au kumtenga. Unaweza kufikiria kuendelea kuvuja kwa mkojo au kinyesi ina maana gani kwa mtu binafsi. Matokeo mengine ya fistula ni pamoja na mfadhaiko kila mara, magonjwa ya mwili na maambukizi ya njia ya uzazi, kibofu na figo. Wakati mwingine mwanamke hujiua.

Leba iliyozuiliwa husababisha karibu 20% ya kesi zote za ukuaji wa fistula (Mchoro 9.6).

Matukio = 0.20 x 0.25 x 0.20 = 0.001, au 1 kwa kila 1,000 wanaozaa Mchoro 9.6 Ukadiriaji wa majaribio ya kitaalamkwa maendeleo ya leba ya muda mrefu kwa uzazimfu na utokezaji wa fistula katika nchi zilizo na hatari-kubwa katika nchi za Afrika jangwani mwa Sahara (Chanzo:Amy Tsui and others, The Gates Institute, Johns Hopkins Bloomberg School of Public Health, July 30, 2005).

Katika hali chache, mambo haya yanaweza kusababisha fistula:

  • matatizo ya kuzaliwa: mawasiliano yasiyokuwa ya kawaida kati ya rektamu na uke, inayopatikanawakati wa kuzaliwa
  • maambukizi: hasa kifua kikuu
  • jeraha
  • ngono ya lazima: ubakaji
  • ngono katika umri mdogo

9.5 Matatizo yanayotokana na leba iliyozuiliwa

9.5.2 Matatizo mengine ya kawaida ya leba iliyozuiliwa