9.5.2 Matatizo mengine ya kawaida ya leba iliyozuiliwa
Ikiwa leba iliyozuliwa haitadhibitiwa vizuri, inaweza kusababisha matatizo haya mengine kwa mama:
- Kuvuja damu baada ya kuzaa (utajifunza kuhusu tatizo hili katika Kipindi cha 11)
- Kurudi polepole kwa uterasi kwa hali iliyokuwa kabla ya ujauzito
- Mshtuko (shinikizo la damu la chini na moyo kupiga kwa haraka)
- Utumbo mdogo inapooza na inaacha kusonga(ileus iliyopooza)
- Sepsisi (kuenea kwa maambukizi mwili mzima)
- Kifo
Leba iliyozuiliwa inaweza kusababisha matatizo haya kwa mtoto mchanga:
Unaweza kujifunza kuhusu matatizo yanayowaathiri watoto wachanga katika Moduli ya Utunzaaji baada ya kuzaa na Moduli ya Huduma Sawa kwa watoto wachanga na Magonjwa ya watoto
- Sepsisi kwa mtoto mdogo
- Degedege
- Jeraha usoni
- Ukosefu mkali wa oksijeni (ukosefu wa oksijeni unaotishia maisha)
- Kifo
Back to previous pagePrevious
9.5.1 Fistula