9.6.5 Zuia ndoa ya mapema

Ndoa ya mapema ndio suala la Kipindi cha somo katika Moduli juu ya Vijana Waliobaleghe na Afya ya Uzaaji wa Vijana.

Suala lingine ni ndoa ya mapema. Utafiti katika Sahara ya Afrika imeonyesha kuwa 50% ya wanawake, hasa wale wa vijijini, huolewa katika wastani ya miaka karibu 16. Wengi wa wanawake wadogo hupata mimba haraka. Kikuundi hiki cha kina mama wadogo sana kiko katika hatari hasa ya leba iliyozuiliwa. Pelvisi ya mama wa umri mdogo haijakomaa vilivyo ili kutoshea kichwa cha mtoto. Katika mazungumzo yako na wanawake, wenzio, na viongozi wa jamii, sisitiza hatari za ndoa ya mapema. Jaribu kuwashawishi kuchelewesha kuzaa mtoto wa kwanza mpaka baada ya mwanamke kufikia miaka 18. Kuza njia za kupanga uzazi ili kuchelewesha mimba ya kwanza miongoni mwa wanawake hawa wadogo sana. Ikiwa mimba isiyotarajiwa itatokea, ni muhimu pia kuwashauri kuhusu huduma salama ya utoaji wa mimba (Moduli ya Utunjazi katika Ujauzito, Sehemu ya 2, Kipindi cha 20).

9.6.4 Mafunzo ya lishe bora

Muhtasari wa Kipindi cha 9