Malengo ya Somo la Kipindi cha 10

Baada ya kipindi hiki, utaweza:

10.1 Kufasili na kutumia kwa usahihi maneno yote muhimu yaliyo kwenye herufi nzito. (Maswali ya kujitathmini 10.1 na 10.2)

10.2 Kueleza mambo yanayoongeza hatari ya urarukaji wa uterasi. Kufafanua ni kwa nini wanawake waliozaa zaidi ya mara moja wamo katika hatari kubwa zaidi kuliko wale wanaozaa kwa mara ya kwanza. (Swali la kujitathmini 10.2)

10.3 Kueleza ishara za hatari na ishara za kitabibu za urarukaji wa uterasi. Kueleza matatizo yanayotokea sana kutokana na urarukaji wa uterasi. (Maswali ya kujitathmini 10.3 na 10.4)

10.4 Kufafanua jinsi ya kufanya utatuzi kwa wanawake wanaoraruka uterasi ili kuokoa maisha yao. Kueleza hatua utakazochukua ili kupunguza hatari ya urarukaji wa uterasi katika leba. (Swali la kujitathmini 10.4)

Kipindi cha 10 Uterasi Iliyoraruka

10.1 Mambo yanayoongeza hatari ya urarukaji wa uterasi