10.1 Mambo yanayoongeza hatari ya urarukaji wa uterasi

Ikiwa uzazi umezuilika huku uterasi ikiendelea kunywea, inaweza kuraruka. Tayari unajua kuhusu matatizo ya leba na kuzaa kutoka kwa Vipindi vya 8 na 9. Unapaswa uweze kujibu swali hili.

  • Je, ni mambo yapi yanayoongeza hatari ya urarukaji wa uterasi?

  • Ikiwa leba imezuilika kutokana na visababishi hivi, uterasi inaweza kuraruka:

    • Kutolingana kwa sefalopelvisi: kichwa cha fetasi ni kikubwa sana au pelvisi ya mama ni ndogo sana. Mtoto hawezi kuteremka kwenye njia ya uzazi.
    • Mlalo mbaya wa fetasi au fetasi kutokuwa katika nafasi yake ya kawaida: Kwa mfano, mtoto yuko katika mlalo wa kutanguliza matako, uso, paji la uso au bega. Au mtoto yuko katika mlalo wa kutanguliza veteksi ilhali kisogo chake kiko upande wa nyuma wa mama (Kisogo-nyuma ni kwamba kisogo cha mtoto kiko upande wa nyuma wa pelvisi ya mama.)
    • Ujauzito wa zaidi ya fetasi moja: Pacha au watoto zaidi hasa ikiwa “wameshikamana” shingoni au waliounganika.
    • Kizuizi cha kimaumbile: Kitu kitokanacho na maumbile kuzuia mtoto kuteremka. (Kwa mfano, tyuma kwenye fumbatio au uterasi.)
    • Kovu za uterasi.

    Mwisho wa jibu

Visababishi vinne vya kwanza vimeshajadiliwa kwa kina katika vipindi vya hapo awali. Kipindi hiki kinaeleza kutokea kwa kovu kwenye uterasi na visababishi vingine vya urarukaji wa uterasi.

Malengo ya Somo la Kipindi cha 10

10.1.1 Uterasi yenye kovu