10.1.3 Fistula iliyokarabatiwa hapo awali

Ulisoma kuhusu fistula katika Kipindi cha 9. Fistula ni mojawapo ya matatizo makali ya leba iliyozuiliwa. Fistula imeenea sana katika maeneo ya mashambani barani Afrika. Wakati mwingine, mwanamke hupata fistula katika leba ya hapo awali na kisha ikarabatiwe kwa njia ya upasuaji. Fistula inapopona, kovu kubwa zinaweza kutokea na kuzuia kuzaliwa kwa mtoto atakayefuata.

  • Je, ni sehemu ipi ya njia ya uzazi inayopata kovu kutokana na ukarabati wa fistula?

  • Uke. Fistula ni mwanya unaopasuka katikati ya uke na labda kibofu cha mkojo, rektamu, urethra, au ureta.

    Mwisho wa jibu

Washauri kwa dhati wanawake walio na kovu kwenye uterasi, seviksi, au uke kuzaa mtoto wao atakayefuata katika kituo cha afya. Mwanamke huyu anaweza kuhitaji damu na vyombo vya upasuaji, pamoja na ujuzi wa kufanya upasuaji wa kuzaa.

10.1.2 Seviksi yenye kovu

10.2 Kwa nini wanawake waliozaa zaidi ya mara moja wako katika hatari kubwa ya urarukaji wa uterasi?