10.2 Kwa nini wanawake waliozaa zaidi ya mara moja wako katika hatari kubwa ya urarukaji wa uterasi?

Mwanamke aliyezaa mara mbili au zaidi amezaa angalau mtoto mmoja baada ya majuma 28 ya ujauzito. Umri wa ujauzito ni muhimu. Baada ya majuma 28, fetasi hutimiza ukubwa na uzani halisi. Uterasi ya mwanamke huyu tayari imetanuka. Kuzaa kunatarajiwa kuwa rahisi katika ujauzito utakaofuata. Licha ya ukweli huu, ikiwa leba zao zitazuilika, wanawake waliozaa mara mbili au zaidi wana uwezekano mkubwa wa kukumbwa na urarukaji wa uterasi kuliko wale wanaozaa mara ya kwanza.

  • Je, unaweza kupendekeza sababu ya tokeo hili lisilotarajiwa?

  • Sababu moja ni kuwa kina mama wa mara ya kwanza hawana historia ya hapo awali ya matatizo ya ujauzito. Mwanamke aliyezaa mara mbili au zaidi anaweza kuwa na kovu kwenye uterasi au sehemu zingine za njia ya uzazi. Kovu hizi ni visababishi vya hatari ya urarukaji wa uterasi.

    Mwisho wa jibu

10.1.3 Fistula iliyokarabatiwa hapo awali

10.2.1 Inesha ya uterasi