10.2.1 Inesha ya uterasi

Sababu nyingine ya wanawake waliozaa mara mbili au zaidi walio na leba iliyokaa kwa muda mrefu au iliyozuilika kuwa katika hatari zaidi ya urarukaji wa uterasi ni kuwa wana minyweo mikali ya leba kwa muda mrefu zaidi kuliko wale wanaozaa kwa mara ya kwanza.

Kwa wanawake wanaozaa kwa mara ya kwanza, minyweo ya uterasi huwa mikali kwa takribani saa 24 za kwanza za leba. Baada ya saa 24, minyweo hii hufifia kwa ukali na kuwa mifupi. Baada ya takribani saa 36, uterasi imeishiwa nguvu. Wanawake hawa wanaozaa kwa mara ya kwanza hupata inesha ya uterasi. Ukali wa minyweo hii hufifia kabisa. Minyweo hii hudumu kwa muda mfupi na kutenganishwa na muda mrefu baina ya mnyweo mmoja na mwingine. Kwa kina mama hawa wa mara ya kwanza, minyweo ya uterasi imekaribia kuisha na kwa hivyo urarukaji wa uterasi ni nadra. Kwa upande mwingine, minyweo ya uterasi kwa wanawake waliozaa zaidi ya mara moja hubaki mikali, thabiti na ya mara kwa mara kwa muda mrefu zaidi. Wanawake waliozaa zaidi ya mara moja wanapokuwa katika leba, kuna uwezekano mkubwa wa kuraruka kwa uterasi.

Wanawake wanaozaa kwa mara ya kwanza hukumbwa na matatizo mengine makali. Inesha ya uterasi humaanisha kusalia kwa kichwa cha fetasi kwenye pelvisi ya mama kwa muda mrefu. Hatari ya hipoksia ya fetasi huongezeka, ambayo ni uhaba wa oksijeni kwa fetasi. Hatari ya kutokea kwa fistula huongezeka, ambayo husababisha ubakizaji wa mkojo na maambukizi kwenye kibofu cha mama kilichozuilika.

10.2 Kwa nini wanawake waliozaa zaidi ya mara moja wako katika hatari kubwa ya urarukaji wa uterasi?

10.2.2 Usingaji wa kiasili wa fumbatio