10.2.2 Usingaji wa kiasili wa fumbatio

Katika sehemu fulani za Afrika, usingaji wa fumbatio katika leba ni tendo la kawaida la kijamii. Usingaji wa fumbatio hufanywa sana leba inapokaa kwa muda mrefu. Wakunga au wanawake wa kijiji hutumia siagi na mafuta ya kulainisha kusugua fumbatio. Wao huminya fandasi ya uterasi ili kujaribu kumsukuma mtoto upande wa chini. Kitendo hiki cha kijamii ni cha kudhuru sana. Usingaji wa fumbatio unaweza kusababisha urarukaji wa uterasi hasa kwa wanawake waliozaa zaidi ya mara moja.

10.2.1 Inesha ya uterasi

10.2.3 Utumiaji mbaya wa vichochelezi vya toni ya uterasi