10.2.3 Utumiaji mbaya wa vichochelezi vya toni ya uterasi

Ili kudhibiti kipindi cha tatu cha leba, unaweza kutumia dawa ya toni ya uterasi, ambayo huifanya uterasi kunywea. (Dawa hizi ni misoprostol, oxytocin au ergometrine. Zote zimeelezewa kwa kina katika Kipindi cha 6.) Kabla ya kupeana dawa ya toni ya uterasi, hakikisha kuwa uterasi haina fetasi nyingine. Ukimpa dawa ya toni ya uerasi kukiwa na fetasi ndani ya uterasi, uterasi hii inaweza kuraruka na mtoto kupata asfiksia.

  • Je, kwa nini kina mama waliozaa zaidi ya mara moja wamo katika hatari zaidi ya kuraruka kwa uterasi kuliko wenzao wanaozaa mara ya kwanza?

  • Kovu kwenye uterasi ni kisababishi kikuu cha hatari kwa urarukaji wa uterasi. Tishu ya kovu si nyumbufu sana na inaweza kuraruka minyweo inapotokea. Mwanamke aliyezaa zaidi ya mara moja anaweza kuwa na kovu kutokana na upasuaji wa kuzaa au uzazi wenye matatizo ulioijeruhi njia ya uzazi. Uterasi yake pia hunywea kwa muda mrefu. Mwanamke huyu hapati inesha ya uterasi hata ikiwa leba imezuilika.

    Mwisho wa jibu

10.2.2 Usingaji wa kiasili wa fumbatio

10.3 Ishara za kitabibu na athari za urarukaji wa uterasi