10.3.1 Ishara za hatari za uterasi inayoelekea kuraruka

Jedwali 10.1 linaonyesha ishara za hatari zinazotokea sana uterasi inapoelekea kuraruka. Ishara hizi ndivyo viashiria bora zaidi kuwa leba imezuilika na kuwa uterasi inaweza kuraruka karibuni. Urarukaji unaweza kutokea ila mtoto azaliwe haraka kwa njia ya upasuaji.

Kisanduku 10.1 Ishara za hatari za kuraruka kwa uterasi

  • Minyweo mikali na ya mara kwa mara ya uterasi inayotokea zaidi ya mara 5 kwa kila dakika 10 na/ au kila mnyweo kudumu kwa sekunde 60 - 90 au zaidi.
  • Kiwango cha mpigo wa moyo wa fetasi kilicho juu ya mipigo 160 kwa dakika au chini ya mipigo 120 kwa dakika, kinachoendelea kwa zaidi ya dakika 10. Ishara hii, mara nyingi, ndiyo huwa ya kwanza kabisa kuonyesha kuwa kuzuilika kunaiathiri fetasi.
  • Kutengenezwa kwa kizingo cha Bandl (Kipindi cha 9 na Mchoro 10.1).
  • Maumivu kwenye sehemu ya chini ya uterasi.
  • Kotokwa na damu ukeni kunaweza pia kuashiria kuraruka kwa uterasi.
Mchoro 10.1 Umbo la kawaida la fumbatio (upande wa kushoto) na uterasi iliyozulika iliyo na kizingo cha Bandl (upande wa kulia), ambacho ni kiashiria cha hatari ya urarukaji unaoelekea.
  • Je, patografu inawezaje kukusaidia kujua kuwa uterasi inaelekea kuraruka?

  • Tumia patografu kuchora idadi ya marudio na muda ambao minyweo itadumu. Chora mabadiliko kwa kiwango cha mpigo wa moyo wa fetasi. Kwa hivyo utagundua haraka ikiwa mojawapo ya idadi hizo zipo katika eneo la hatari lililoonyeshwa katika Jedwali 10.1.

    Mwisho wa jibu

10.3 Ishara za kitabibu na athari za urarukaji wa uterasi

10.3.2 Ishara Zinazoonyesha kuwa uterasi imeraruka