10.3.2 Ishara Zinazoonyesha kuwa uterasi imeraruka

Ishara ya kwanza kuwa uterasi imeraruka ni kukoma kabisa kwa minyweo ya uterasi. Dalili zingine hufuata haraka.

Fumbatio lililofura na lenye maumivu

Maumivu haya huhisika unapoligusa fumbatio. Fumbatio lina maumivu kwa sababu ya kuraruka kwa uterasi na kero lisababishwalo na damu inayojikusanya kwenye kaviti ya fumbatio. Fumbatio linaonekana kuwa lililofura kwa sababu uterasi imejifunga kwa mwili wa fetasi na damu kumwagika ndani ya kaviti ya fumbatio. Kusonga kwa utumbo kumepungua au kumekoma, na kwa hivyo huwezi kusikia sauti za kusonga kwa utumbo kwa stethoskopu. (Kusonga kulikopungua au kulikokoma kwa utumbo huitwa enteroflejia.) Kibofu pia kinaweza kuzuilika, hali inayochangia kufura na maumivu. Muda unaposonga, maambukizi yanaweza kukua kwenye fumbatio na kusababisha kufura zaidi.

Sehemu za fetasi zinazoweza kutomasika kwa urahisi, fetasi kutosonga, na sauti za mpigo wa moyo wa fetasi

Fetasi haiwezi kuishi kwa muda mrefu ndani ya uterasi iliyoraruka. Kwanza, uterasi hujifunga kwa mkazo kwenye mwili wa fetasi. Kisha sehemu fulani za fetasi zinaweza kupita kwenye mikato. Au fetasi nzima iweze kupita hadi kwenye kaviti ya fumbatio. Ukitomasa fumbatio, ni ukuta wa fumbatio tu ulio katikati ya mkono wako na fetasi. Kwa hivyo, unaweza kuhisi sehemu za fetasi kwa urahisi. Ikiwa mtoto amefariki, mama hawezi kumhisi akisonga na huwezi kusikia mpigo wa moyo wake.

10.3.1 Ishara za hatari za uterasi inayoelekea kuraruka

10.3.3 Athari kwa mama