10.4 Utatuzi wa uterasi iliyoraruka

Tumia miongozo hii ili kuzuia au kupunguza hatari ya kuraruka kwa uterasi kwa wanawake walio katika leba:

  • Tumia patografu kufuatilia kuendelea kwa mwanamke aliye katika leba. Patografu huhakikisha kuwa unapata dalili mapema ikiwa leba haitaendelea kikawaida. (Ulisoma jinsi ya kutumia patografu katika Kipindi cha 4).
  • Wape wanawake rufaa haraka ukishuku kuwa leba imekaa sana au imezuilika.
  • Wanawake waliozaa zaidi ya mara moja wanaweza kuwa na kovu kwenye uterasi kutokana na matatizo ya uzazi wa hapo awali. Washauri wazalie katika kituo cha afya ambapo wanaweza kutiwa damu na kufanyiwa upasuaji. Toa ushauri huu kwa mwanamke yeyote aliyetolewa tyuma kwenye uterasi.
  • Waeleze wanajamii kwa nini kutosinga uterasi ni muhimu wakati wa leba au kutoweka shinikizo kwenye uterasi ili kujaribu kuharakisha uzazi. Waambie wasifanye msingo huu hata ingawa ni mazoea ya kiasili.
  • Tumia dawa za toni ya uterasi kusaidia kutoa plasenta lakini tu baada ya kuhakikisha kuwa fetasi ya mwisho imezaliwa.

10.3.3 Athari kwa mama

10.4.1 Kigezo cha rufaa kwa leba iliyokaa sana