10.4.1 Kigezo cha rufaa kwa leba iliyokaa sana

Usiache mwanamke akawie katika kipindi cha kwanza au cha pili cha leba kwa muda mrefu. Wape wanawake hawa rufaa haraka.

  • Je, ni lini unapopaswa kumpa rufaa mwanamke aliyezaa zaidi ya mara moja au anayezaa kwa mara ya kwanza ambaye leba yake imekaa kwa muda mrefu? (Kumbuka Kipindi cha 9.)

  • Wape rufaa wanawake walio na ishara hizi za leba iliyokaa sana:

    • Kipindi cha kwanza cha leba fiche kinachokaa zaidi ya saa 8 kabla ya kuingia katika kipindi cha kwanza cha leba dhahiri.
    • Kipindi cha kwanza cha leba dhahiri kinachokaa zaidi ya saa 12 kabla ya kuingia katika kipindi cha pili.
    • Kipindi cha pili cha leba kinachokaa zaidi ya saa moja kwa wanawake waliozaa zaidi ya mara moja au zaidi ya saa mbili kwa wanawake wanaozaa kwa mara ya kwanza, ila kuzaa kunaelekea kutendeka.

    Mwisho wa jibu

Wajibu wako mkuu ni uzuiaji wa kimsingi. Hakikisha kuwa iwapo leba itazuilika, unaweza kumpeleka mwanamke huyu katika kituo cha afya apate utunzaji wa dharura kwa wakati unaofaa ili kuzuia kuraruka kwa uterasi. Hata hivyo, sababu nyingi zinaweza kuhitaji kuwa umpe mwanamke aliye na uterasi iliyoraruka utunzaji wa dharura. Kisha jukumu lako ni uzuiaji wa baadaye wa maambukizi yanayohusiana na urarukaji wa uterasi.

10.4 Utatuzi wa uterasi iliyoraruka

10.4.2 Uzuiaji wa kimsingi: fika katika kituo cha afya kwa utunzaji wa dharura kabla ya uterasi kuraruka