10.4.2 Uzuiaji wa kimsingi: fika katika kituo cha afya kwa utunzaji wa dharura kabla ya uterasi kuraruka
Kumbuka ulichosoma katika moduli ya utunzaji katika ujauzito (Kipindi cha 13) na majadiliano kuhusu jinsi ya kutoa rufaa. Je, ni nini unachopaswa kukumbuka kufanya?
Fanya mambo haya unapotoa rufaa:
- Andika barua ya rufaa iliyo na habari nyingi iwezekanavyo.
- Andaa mpango wa dharura wa usafirishaji wa jamii kwa mama huyu. Ukiweza, enda naye.
- Ikiwezekana, wajulishe wahudumu katika kituo hicho cha afya wamtarajie mama huyu. Vituo vingi vya afya vinaweza kuwa katika umbali sawa. Tambua ni kituo kipi kinachoweza kumfanyia upasuaji wa dharura na kumwongeza damu na kisha umtume huko.
Mwisho wa jibu
Back to previous pagePrevious
10.4.1 Kigezo cha rufaa kwa leba iliyokaa sana