10.4.3 Uzuiaji wa baadaye: utunzaji wa dharura kwa mwanamke aliye na mshtuko

Mwanamke aliye kwenye mshtuko anahitaji usaidizi wa haraka. Mtibu haraka ili kuokoa maisha yake.

Mshtuko ni athari isiyoepukika ya uterasi iliyoraruka. Mpe rufaa haraka aende katika kituo cha afya kilicho karibu chenye huduma zinazofaa za utunzaji wa dharura. Njiani, hakikisha kuwa mwanamke amelala miguu yake ikiwa juu kidogo kuliko kichwa chake na kichwa chake kimekunjwa kuelekea upande mmoja (Mchoro 10.2). Hakikisha anapata joto na ametulia.

Mchoro 10.2 Namna ya kumsafirisha mwanamke aliye kwenye mshtuko kwenda hospitalini. Mfunike kwa blanketi ili apate joto.

Ikiwa umefundishwa kufanya haya, anza kwa kumpa viowevu mishipani. Ulisoma jinsi ya kufanya hivi katika Moduli ya utunzaji katika ujauzito, Kipindi cha 22 na katika mafunzo yako ya ujuzi tendaji. Ikiwa ana fahamu, anaweza kunywa maji au viowevu vya kumwongezea maji (chumvi za mdomoni za kuongeza maji). Ikiwa hana fahamu, usimpe kitu chochote mdomoni. Usimpe dawa, kinywaji au chakula.

Unafaa kuwa ulishatimiza matayarisho haya:

  • Hakikisha kuwa ushauri wako wakati wa ujauzito ulimfafanulia kinaganaga jinsi ilivyo muhimu kupata usaidizi maalum anapoenda katika leba.
  • Shawishi familia na jamii ya mwanamke huyu kupangia dharura zinazoweza kutokea. Msaada wa kifedha na usafiri unaweza kuhitajika.
  • Hakikisha kuwa unaweza kufanya utambuzi wa mapema na ufanye taratibu za dharura kabla ya rufaa.
  • Hakikisha kuwa watu wawili wazima wenye afya wanaoweza kumtolea damu wameenda naye. Enda naye ukiweza.

Hatimaye jaribu kupunguza kuchelewa, jambo linaloweza kuwa ndilo tofauti kati ya uhai na mauti. Wanawake wengi waafrika hufariki kutokana na urarukaji wa uterasi kwa sababu wanasita kutafuta usaidizi maalum wakati wa kuzaa. Kisha wanachelewa kutafuta usaidizi wa kimatibabu baada ya urarukaji wa uterasi. Matibabu yanacheleweshwa zaidi kwa sababu ya umbali wa kituo cha afya au ukosefu wa vifaa na wahudumu mwanamke anapofika kwa utunzaji wa dharura.

Kumbuka mambo haya yote ili kuhakikisha kuwa mwanamke huyu amepewa rufaa ya kwenda katika kituo mwafaka haraka kwa utatuzi na utunzaji wa dharura.

10.4.2 Uzuiaji wa kimsingi: fika katika kituo cha afya kwa utunzaji wa dharura kabla ya uterasi kuraruka

Muhtasari wa Kipindi cha 10