Muhtasari wa Kipindi cha 10

Katika Kipindi cha 10, ulisoma yafuatayo:

  1. Barani Afrika, urarukaji wa uterasi mara nyingi hutokana na kupuuzwa kwa leba iliyozuilika. Kwa utatuzi wa mapema na utunzaji ufaao, urarukaji wa uterasi unaweza kuzuiliwa.
  2. Visa zaidi vya urarukaji wa uterasi hutokea kwa wanawake waliozaa zaidi ya mara moja kuliko wale wanaozaa kwa mara ya kwanza. Sababu moja ni kuwa, kwa wanawake wanaozaa kwa mara ya kwanza, inesha ya uterasi hutokea. Inesha ya uterasi hupunguza nguvu na marudio ya minyweo isababishayo kuraruka kwa uterasi.
  3. Inesha ya uterasi kwa wanawake wanaozaa mara ya kwanza ina hatari zingine: Kichwa cha fetasi hukawia kwenye pelvisi kwa muda mrefu. Hatari ya hipoksia ya fetasi, kuanza kwa fistula, mkojo kubakizwa na maambukizi kwenye kibofu kiko juu sana.
  4. Kisababishi kikuu cha urarukaji wa uterasi ni leba iliyozuilika. Leba iliyozuilika husababishwa na kutolingana kwa sefalopelvisi, mlalo mbaya au fetasi kutokuwa katika nafasi yake ya kawaida, ujauzito wa zaidi ya mtoto mmoja, tyuma kwenye uterasi, au kovu. Mambo mengine yaongezayo hatari ya urarukaji wa uterasi ni fistula iliyokarabatiwa hapo awali, utumizi mbaya wa dawa za toni ya uterasi na usingaji wa fumbatio na wakunga wa kiasili katika leba.
  5. Ishara za kitabibu za uterasi inayoelekea kuraruka ni minyweo ya uterasi inayoendelea kutokea na inayodumu kwa muda wa sekunde 60-90 au zaidi, minyweo inayotokea zaidi ya mara 5 kwa kila dakika 10, na mpigo duni wa moyo wa fetasi. (Mpigo wa moyo wa fetasi unaoendelea kuwa juu ya mipigo 160 kwa dakika au chini ya mipigo 120 kwa dakika.) Dalili zingine ni kutokea kwa kizingo cha Bandl, maumivu kwenye fumbatio ukitomasa na pengine kutokwa na damu ukeni.
  6. Kukoma kabisa kwa minyweo ndiyo ishara muhimu zaidi ya kuwa uterasi imeraruka.
  7. Ishara zingine za uterasi iliyoraruka zinaweza kuwa maumivu kwenye fumbatio ukitomasa, sehemu za fetasi zinazotomasika kwa urahisi, kuvimba kwa fumbatio, kutosonga kwa fetasi na kutokuwepo kwa mpigo wa moyo wa fetasi.
  8. Hali ya kiafya ya mwanamke mwenye uterasi iliyoraruka hutegemea kiasi cha damu iliyopotea, muda tangu iliporaruka na kuwepo kwa maambukizi yaliyokithiri.
  9. Matatizo yatokeayo sana ya urarukaji wa uterasi ni kifo cha fetasi, na cha mama, maambukizi na mshtuko utokanao na upotezaji wa damu na/au sepsisi, peritonitisi, figo kutofanya kazi na upasuaji wa kutoa uterasi.
  10. Baadhi ya sababu za kufariki kwa wanawake wengi waafrika kutokana na urarukaji wa uterasi ni: kusita kutafuta usaidizi maalum wakati wa kuzaa na kisha kuchelewa kutafuta usaidizi wa kimatibabu baada ya uterasi kuraruka; kuchelewa zaidi katika kupata matibabu kwa sababu ya urefu wa safari ya kufikia kituo cha afya; au ukosefu wa vifaa na wahudumu waliohitimu mwanamke huyu anapofika kwa utunzaji wa dharura.

10.4.3 Uzuiaji wa baadaye: utunzaji wa dharura kwa mwanamke aliye na mshtuko

Maswali ya Kujitathmini ya Kipindi cha 10