Maswali ya Kujitathmini ya Kipindi cha 10

Kwa kuwa umekamilisha kipindi hiki, jibu maswali haya ili kutathmini ulivyosoma. Unaweza kulinganisha majibu yako na Muhtasari juu ya Maswali ya Kujithmini mwishoni mwa Moduli hii.

Swali la kujitathmini 10.1 (linatathmini Malengo ya Somo la 10.1 na 10.2)

Ni mambo yapi yanayoweza kumfanya mwanamke apate urarukaji wa uterasi?

Answer

Mambo haya yanaongeza hatari ya kuraruka kwa uterasi: (Maneno muhimu yako kwenye herufi nzito.)

  • Leba iliyozuilika kutokana na: kichwa cha fetasi kuwa kikubwa zaidi au pelvisi ya mama kuwa ndogo zaidi (kutolingana kwa sefalopelvisi); mtoto kutoweza kuteremka kwenye njia ya uzazi; mlalo mbaya na fetasi kutokuwa katika nafasi yake; au ujauzito wa zaidi ya mtoto mmoja (Kipindi cha 8).
  • Vizuizi vingine vya kimaumbile kama vile tyuma au kovu kutokana na uzazi wa hapo awali. (Kwa mfano, fistula, ambao ni mkato kati ya uke na kibofu, rektamu, urethra au ureta.)
  • Mazoea ya kiasili kama vile msingo usiofaa wa fumbatio au kusukuma chini kwenye fandasi katika leba.
  • Utumiaji mbaya wa dawa ya toni ya uterasi. (Dawa hii hutumiwa kusababisha minyweo.)

Mwisho wa jibu

Swali la kujitathmini 10.2 (linatathmini Malengo ya Somo la 10.1 na 10.2)

Kwa nini wanawake waliozaa zaidi ya mara moja wako katika hatari kubwa ya urarukaji wa uterasi kuliko wale wanaozaa mtoto wa kwanza?

Answer

Wanawake wanaozaa mtoto wa kwanza wanazaa kwa mara ya kwanza. Katika uzazi wa kwanza, kuna uwezekano wa leba kuwa ndefu. Hata hivyo, kwa wanawake hawa, inesha yauterasi hutokea baada ya takribani saa 36. Minyweo huwa dhaifu na mifupi, na yenye muda mrefu baina yake. Inesha ya uterasi hupunguza hatari ya urarukaji wa uterasi kwa kiwango kikubwa .

Kwa upande mwingine, wanawake waliozaa zaidi ya mara moja wamepata angalau mtoto mmoja baada ya majuma 28 ya ujauzito. Uterasi ya wanawake hawa hunywea mno kwa muda mrefu zaidi kuliko uterasi ya wale wanaozaa kwa mara ya kwanza. Ikiwa uzuio utazuia kuzaa kwa muda mrefu, hasa ikiwa kuna kovu kutokana na matatizo ya uzazi wa hapo awali, kuna uwezekano mkubwa wa uterasi kuraruka.

Mwisho wa jibu

Swali la kujitathmini 10.3 (linatathmini Malengo ya Somo la 10.3)

Kamilisha Jedwali 10.1. Ongeza maelezo ya dalili za hatari za urarukaji wa uterasi unaoweza kutokea.

Jedwali 10.1 Dalili za hatari za uwezekano wa urarukaji wa uterasi.
Hatua Dalili za hatari
Pima muda wa vipindi vya leba
Pima minyweo ya uterasi
Chunguza kiwango cha mpigo wa moyo wa fetasi
Chunguza fumbatio
Chunguza uke

Answer

Jedwali 10.1 lililokamilishwa ndilo hili hapa.

Jedwali 10.1 Dalili za hatari ya uwezekano wa urarukaji wa uterasi (iliyokamilishwa
Hatua Dalili za hatari
Pima muda wa vipindi vya lebaLeba ndefu sana: kipindi cha kwanza cha awamu fiche kinadumu zaidi ya saa18; kipindi cha kwanza cha awamu ya leba dhahiri kinadumu zaidi ya saa 12; kipindi cha kinadumu zaidi ya saa 1 kwa wanawake waliozaa zaidi ya mara moja, au zaidi ya saa 2 kwa wanawake wanaozaa kwa mara ya kwanza
Pima minyweo ya uterasi Minyweo ya uterasi inayoendelea kutokea inayodumu kwa muda wa sekunde 60 - 90 au zaidi, inayotokea zaidi ya mara 5 kwa kila dakika 10
Chunguza kiwango cha mpigo wa moyo wa fetasiKiwango cha mpigo wa moyo wa fetasi kinaendelea kuwa zaidi ya mipigo 160 kwa dakika au chini ya mipigo 120 kwa dakika
Chunguza fumbatioSehemu ya chini ya uterasi ni nyororo ukitomasa; kizingo cha Bandl kipo
Chunguza ukeKunaweza kuwa na kutokwa na damu

Mwisho wa jibu

Swali la kujitathmini (linatathmini Malengo ya Somo la 10.3 na 10.4)

  • a.Ni matatizo gani yanayoweza kufuata urarukaji wa uterasi?
  • b.Ni hatua zipi unazopaswa kuchukua iwapo urarukaji wa uterasi utatokea?

Answer

  • a.Matatizo ya urarukaji wa uterasini:
    • Kifo cha fetasi ila upasuaji wa haraka ufanywe kuitoa.
    • Mama kutokwa na damu nyingi na kupatwa na mshtuko kutokana na upotezaji huu wa damu, ambayo husababisha kifo cha mama ila apate matibabu ya haraka. (Kutokwa na damu nyingi sana na mshtuko utokanao na upotezaji huu wa damu hutambulika kwa upotezaji wa fahamu, ngozi kukwajuka, mpwito wa haraka wa ateri, shinikizo la damu linalopungua, upumuaji wa haraka, kuanza kupoteza fahamu na utoaji wa kiasi kidogo cha mkojo.)
    • Maambukizi: peritonitisi (maambukizi ya kaviti ya fumbatio) na/au septisemia (maambukizi ya damu yatokanayo na bakteria), ambayo husababisha uwezekano wa mshuto wa sepsisi unaoweza kusababisha kifo.
    • Figo kukosa kufanya kazi (kwa sababu ya kupoteza kiasi cha damu).
    • Histeroktomi.
  • b.Hatua muhimu zaidi ni kumpeleka mwanamke huyo katika kituo cha afya kilicho karibu kinachoweza kutibu uterasi iliyoraruka haraka iwezekanavyo. Hakikisha anapata joto na ametulia. Anafaa kulala miguu yake ikiwa juu kidogo kuliko kichwa chake na kichwa chake kikiwa kimekunjwa kuelekea upande mmoja. Mpe viowevu mshipani. Ikiwa hana fahamu, usimpe chochote mdomoni.

Mwisho wa jibu

Muhtasari wa Kipindi cha 10