Malengo ya Somo la Kipindi cha 11

Baada ya kipindi hiki, unatarajiwa:

11.1 Kufasili na kutumia kwa usahihi maneno yote muhimu yaliyoandikwa kwa herufi nzito. (Swali la Kujitathmini 11.1)

11.2 Kueleza visababishi na vipengele hatari vya hali ya kuvuja damu baada ya kuzaa inayohusiana na jeraha na uterasi kutojikaza vyema. (Swali la Kujitathmini 11.2)

11.3 Kueleza hatua zinazoweza kusaidia kuzuia kuvuja damu baada ya kuzaa. Jumuisha hatua utakazochukua wakati wa ujauzito na awamu ya pili na tatu ya leba. (Swali la Kujitathmini 11.3)

11.4 Kufafanua jinsi ya kudhibiti hali ya dharura katika wanawake wanaovuja damu baada ya kuzaa. (Swali la Kujitathmini 11.3)

Kipindi cha 11 Kuvuja Damu baada ya Kuzaa

11.1 Kuvuja damu baada ya kuzaa ni nini?