11.1 Kuvuja damu baada ya kuzaa ni nini?

Kuvuja damu baada ya kuzaa ni hali ya kuvuja damu kupita kiasi kutoka kwenye njia ya mfumo wa uzazi wakati wowote baada ya kuzaa hadi wiki sita baadaye. Takriban asilimia 70-90 ya matukio ya hali hii hutokea wakati wowote katika saa 24 za kwanza baada ya kuzaa. Matukio haya hutokea kwa sababu uterasi haikujikaza vyema baada ya plasenta kutengeka. Mikazo dhabiti ni muhimu ili kuziba mishipa ya damu kwenye shina la plasenta.

Vipengele hatari ni hali zilizopo zinazofanya hali hii kuwa, na uwezekano wa juu wa kutokea au kuwa na hatari zaidi kwa hali hii.

Kuvuja damu baada ya kuzaa ni hali isiyotabirika na ya kasi inayosababisha vifo vya kina mama. Hali hii haitabiriki kwa sababu thuluti mbili ya wanawake waliokabiliwa na tatizo hili hawana vipengele vya hatari vinavyojulikana. (Kiwango hatari cha hali hii hujulikana na madaktari kama hali idiopathiki ikiwa kisababishi chake hakijulikani.) Katika matukio mengine, wanawake wanaovuja damu baada ya kuzaa huwa na mojawapo au zaidi ya vipengele vya hatari vinavyojulikana. Au damu huvuja kwa sababu mhudumu wa kiafya ameidhibiti vibaya awamu ya tatu ya leba. (Tutavidurusu vipengele vya hatari baadaye katika kipindi hiki.)

Malengo ya Somo la Kipindi cha 11

11.1.1 Ni kiwango gani cha kuvuja damu kilicho cha “kupita kiasi”?