11.1.1 Ni kiwango gani cha kuvuja damu kilicho cha “kupita kiasi”?

Ulijifunza jinsi ya kupima shinikizo la damu na mrindimo katika Kipindi cha 9 cha Moduli ya Utunzaji wa Wakati wa Ujawazito. Tulijifunza kuhusu visababishi na jinsi ya kudhibiti mshtuko unaohusiana na kuvuja damu katika Kipindi cha 20–22 cha Moduli hiyo.

Kwa kawaida, mama hupoteza kiwango kidogo cha damu wakati wa kuzaa. Mama kwa kawaida hupoteza takriban mililita 150 (kikombe 1), za damu wakati wa kuzaa na baada ya plasenta kutolewa. Ikiwa kiwango hiki kitazidi mililita 300 (vikombe 2), hali hii inaaminiwa kuwa kuvuja damu kupita kiasi (Mchoro 11.1) Kuvuja damu kupita kiasi hufasiliwa kama kuvuja damu zaidi ya mililita 500. Hata hivyo, kwa wanawake wenye anemia kali, kuvuja damu ya hata mililita 200–250 kunaweza kusababisha kifo. Kwa sababu hiyo, ufasili bora zaidi wa kuvuja damu baada ya kuzaa ni " kiwango chochote cha kuvuja kinachosababisha hali ya mwanamke kudhoofika na kusababisha dalili za mshtuko unaohusiana na kuvuja damu." (Dalili hizi ni shinikizo la chini la damu, mrindimo wa kasi, kuparara, unyonge, au utatanishi.)

Mchoro 11.1 Kuvuja damu kwa wingi ni zaidi ya mililita 300; Kuvuja damu kupita kiasi ni zaidi ya mililita 500.

11.1 Kuvuja damu baada ya kuzaa ni nini?

11.1.2 Uainishaji wa kuvuja damu baada ya kuzaa